Jumapili, 27 Novemba 2016

Jigundue!

Mtoto akizaliwa ni mgeni katika dunia kwa hivyo hayajui mambo mengi na hujifunza kila siku iitwapo leo hata uzee wake pengine aweza kosa kuyajua mengine katika siku za uhai wake.

Kujifunza kwake kwatokana na mazingira ambayo wazazi wake wanamchagulia kuishi. Mazingira haya hubadilika kwa sababu kadhaa moja wapo ikiwa ni kuhama kwa familia yake kutoka mahali kwenda mahali pengine.

Mazingira yakuishi yanajumuisha watu na shughuli za watu husika, hali ya hewa na maliasili.

Katika mazingira hayo mtoto huwekwa katika nafasi ya kujigundua ambapo hutambua mambo mbalimbali kuhusu yeye hususani vitu anavyopendelea na asivyopendelea, aina za marafiki, mazingira rafiki, shughuli rafiki na mambo mengi zaidi. Yote ajifunzayo na kuyagundua ndio unaotazamiwa kuwa mtindo wake wa maisha.

Kujitambua ni muhimu katika maisha ya mwanadamu yeyote ili kuepukana na migogoro binafsi katika kufanya maamuzi. Kujitambua kwaongeza idadi ya watu wenye misimamo isiyo pepesuka zaidi tena watu wenye maono na malengo thabiti katika eneo lake.

Mwanzo wa kila badiliko la kijamii ni mtu mmoja aliyedhamiria kuwa chanya na kujigundua yeye mwenyewe kunako mjengea misingi ya maisha ambayo kwa hio hutenda na kuenenda.

Fanya leo, jigundue wapenda nini, na nini hupendi; aina gani ya mziki, aina gani ya maeneo yako unayopendelea kutembelea na kuwepo, na watu wa kuhusiana nao.

JIGUNDUE, JITAMBUE!

Jumatatu, 7 Novemba 2016

Foundations of life.

Basically, most of the things are established upon some elements which are determined to handle the structure in its life time. The structures firmness is based on its established foundations. Therefore, most of the foundations are generated basing on the load that it shall carry.

Foundations are the actions taken today not to be done in future, so protects and guards the future...’

Life has got its foundations; which some in leaser percent are brought up by the influence of the other people and environment and hardly the large percent being personally based. The large percent initiated by man come as a result of which he agrees and what he does not agree to follow; basically from the environment he is situated in.

In building such foundations, man ought to be careful because such foundations shall act as principles to guide him in all his lifetime. Man ought to be sure of the bill to pass by his signature and what neither ink nor art in his mind shall be wrapped upon.

Foundations establishes the guidelines for sound decision making and judgement as well. They define personal protocol, procedures, stability and power; thus shouldn't be exposed easily for pollution. They furthermore, carry the personal identity: which describes your peculiarity and uniqueness!

Guard the foundations so serious, so careful; their fall is your life conclusion.

Jumatano, 19 Oktoba 2016

Ujasiri kama Tembo mbele ya Simba!

Soma na mshirikishe na mwingine!

Upo wakati ambao mtu huchoka, pia upo wakati amabao mtu hukata tamaa, upo wakati ambao tumaini huondoka na ngome ya imani huanguka...

Hizi ni nyakati ambazo kila mwanadamu anapitia na wala si wewe peke yako...

Yanayokusonga si kuwa ni mlima usiofaa kuukwea hata kilele chake na kuufikia upande wa pili, tena si ukuta usioweza kubomolewa na kuufikia upande wa pili, si mto usiofaa kuogelea hata kuifikia ngambo yake, tena si kwamba ni jambo ambalo halijawahi kutokea hapo kale; La Hasha! Lakini yote yamekwisha kuwako japo kwa sasa yaweza kuwa na sura tofauti lakini kusudi na dhamira ndani yake ni ile ile...

Je, umejitazama katika kioo na kuona vile jambo lako lilivyo dogo na la kawaida sana? Unakosea kulitafakari ilihali wapaswa kuona njia ya kupita humo. Badili tu mtazamo wako na kuiona changamoto hio kama jiwe la mchanga wa jangwani ambalo hata kwa kulipuliza kwa hewa ya kinywa chako linasambaa.

Wahitaji si nguvu nyingi ila kidogo tu kulikabili jambo hili fanya kuruhusu sehemu ya wewe ambayo haijawahi onekana kudhihirika katika matendo. Kuwa jasiri kama Tembo mbele ya Simba! Amua leo kutumia mwili wako kwa ukubwa wake na uzito wote na ndovu ulizo nazo kumkabili Simba ambaye mwili wake ni mdogo na silaha zake pekee ni meno na miguu basi hana kingine. Kama Tembo waweza kata mti kwa kutumia mkonga wako na kumpiga Simba ambaye hato stahimili maumivu hayo, sharti akimbie tu! Na tangu hapo Tembo kwa heshima hii atakuwa mfalme wa porini.

Shida yako ni ndogo sana sema sifa yake na muonekano wake pamoja na kujigamba kwake na kutamba kwake kunaifanya iwe ya pekee japo ni ya kawaida. Waweza simama leo na kuvunja rekodi kwa kuishinda hali yako. Simama, pigana na uutwae utukufu ambao kwa huo wewe utakuwa mfalme kwa hali hio; mwenye kuheshimika sana na sifa yako kuenea kila mahali toka nchi hata mbingu!

Tangu hapo utaishi maisha ya ushindi na thamani yake ni kubwa kushinda fedha na vito vya thamani.

Na. Mr. Nathanael Kiyuga.